![]() |
| Angalia eneo la mradi kwa kutumia Google maps |
![]() |
Mradi wa Jamii na Utalii Ikolojia Magoroto Mlinga
Lengo kuu la Mradi wa Jamii na Utalii Ikolojia Magoroto Mlinga (MAMCEP) ni kuhifadhi na kuimarisha matumizi endelevu ya misitu ya Magoroto Mlinga katika milima ya Usambara Mashariki, Tanzania. Mradi unaihamasisha jamii inayozunguka misitu hii, ili kijijengea uwezo katika nyanja za uhifadhi wa misitu, kilimo endelevu na kuendeleza shughuli za utalii ikolojia kama njia rafiki na mbadala za kuendeleza maisha yao ya kila siku bila kuathiri kwa kiwango kikubwa mali asili zinazowazunguka. Kipaumbele muhimu kikiwa ni ”uhifadhi wa mmea aina ya Dughulushi (Saintpaulia)” kama nembo au alama ya kuwepo kwa misitu hii. Mradi pia unajishughulisha na shughuli zifuatazo:
- Kuwafundisha na kuwawezesha wanavijiji kujijengea uwezo na mibadala mbalimbali ya kuhifadhi misitu na kilimo endelevu
- Kutekeleza kwa vitendo njia mbalimbali za kilimo endelevu
- Upandaji miti
- Kutambua na kutathmini maeneo yenye mimea aina ya dughulushi, ikiwa ni pamoja na kutambua uhalisia (unasaba) na uwingi wa mimea hii
- Mafunzo ya utalii kwa wanavijiji
- Kutambua vivutio na kuendeleza maeneo ya kitalii
- Kuanzisha na kweka miundombinu ya utalii
- Kuziwezesha taasisi mbalimbalu za wanavijiji ili ziweze zijijengee uwezo wa kujishughulisha na shughuli za hifadhi na utalii na
- Kuutangaza utalii nje na ndani ya maeneo yao.
Taasisi tunazoshirikiana:
Ofisi ya Misitu Hifadhi Mkoa wa Tanga
Halmashauri ya Wilaya Muheza
Mashirika haya yamesaidia mradi kifedha / vifaa:
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |






